Proverbs 3:1-6
Faida Nyingine Za Hekima
1 aMwanangu, usisahau mafundisho yangu,
bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
2 bkwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako
na kukuletea mafanikio.
3 cUsiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe;
vifunge shingoni mwako,
viandike katika ubao wa moyo wako.
4 dNdipo utapata kibali na jina zuri
mbele za Mungu na mwanadamu.
5 eMtumaini Bwana kwa moyo wako wote
wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
6 fkatika njia zako zote mkiri yeye,
naye atayanyoosha mapito yako.
Copyright information for
SwhKC